Inawezekana. Powered by Blogger.

Ujasiriamali na Kilimo cha Mbono

Kilimo cha zao la mbono (Jatropha) sasa ni mkombozi kwa wananchi wa Mpanda.  Ni kama ndoto, lakini huo ndio ukweli halisi kwamba Watanzania tuna raslimali nyingi sana ambazo zinaweza kututoa kimasomaso kiuchumi kama tutaamua kufanya kazi kwa bidii na maarifa na kuwa wabunifu.

Shamba la Mibono

Zao la miti ya mbono kwa wakazi wa maeneo ya Mpanda mkoani Rukwa,limekuwa sasa mkombozi kwa wananchi wa kipato cha chini, hali illiyompelekea Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mizengo Pinda kuwaunga mkono wanachi hao ambao sasa wanazalisha mafuta na sabuni yenye dawa kutokana na zao la mbono.

Mti huu umeweza kuwatoa kimasomaso na kujikuta wakipata mafuta ya taa na dizeli kwa matumizi ya kuendeshea matrekta madogo maarufu kama power tiller.

Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda alifikia uamuzi huo wa kusaidia jumla ya shillingi milioni thelathini (30,000,000) kwa vikundi vya wakulima wa Mpanda ili vijikwamue kwa kutumia teknlogia hiyo rahisi na inayotunza mazingira. Uzinduzi wa mradi wa kukamua mafuta ya dizeli kutoka kwenye mbono ulifanyika mwaka jana wakati wa mbio za mwenge wilayani hapo ambapo mafuta hayo yaliweza kujazwa kwenye magari yaliyokuwa kwenye msafara wa mbio za mwenge.

Unaweza kupata maelezo ya kina zaidi kuhusiana na mradi wa zao la mbono huko Mpanda katika Jarida la Inawezekana toleo la mwezi Juni 2011

Jengo la Mradi wa DISAT huko Mpanda

Post a Comment

About This Blog

  © Blogger template Shush by Ourblogtemplates.com 2009

Back to TOP