Inawezekana. Powered by Blogger.

Kanuni Muhimu za Kuzuia Magonjwa kwa Ndege Wafugwao


  1. Jenga mabanda imara ya kuwasetiri ndege dhidi ya upepo na mvua. Hakikisha mabanda haya yana mzunguko wa hewa safi ya kutosha kwa kuweka madirisha makubwa yenye nyavu. 
  2. Waweke ndege wako ndani ya uzio utakaowazuia ndege wako kuchanganyikana na wengine kutoka nje.
  3. Mabanda ya ndege yafanyiwe usafi mara kwa mara na pia yapuliziwe dawa za kuua wadudu wasumbufu kama viroboto na chawa.
  4. Wingi wa ndege wako lazima uwiane na ukubwa wa mabanda yako. Sio vizuri ndege wako wakisongamana kwenye eneo moja.
  5. Wape ndege wako lishe yenye mchanganyiko wa viini lishe vyote muhimu. Ni vizuri maji safi yakawepo wakati wote.
  6. Tenganisha aina tofauti za ndege, kama kuku, bata, na kadhalika.
  7. Wape ndege wako chanjo za kuzuia magonjwa mbalimbali.
  8. Ndege wagonjwa wanapaswa kutengwa na wazima na wapewe uangalizi wa karibu.
  9. Ndege wanaokufa kwa sababu ya ugonjwa wanapaswa kuchomwa moto au kuzikwa mara moja.
  10. Wapende ndege wako na uwe karibu nao kila inapowezekana. Hii itakusaidia kutambua kwa urahisi magonjwa au matatizo waliyonayo.

Post a Comment

About This Blog

  © Blogger template Shush by Ourblogtemplates.com 2009

Back to TOP