Inawezekana. Powered by Blogger.

MKUTANO WA MASHETANI

Jitahidi usome mpaka mwisho kuna kitu muhimu utajifunza. Toa mawazo yako unavyoona



MKUTANO WA MASHETANI
Lucifer, Mkuu wa mashetani  aliitisha semina elekezi kwa mashetani wote Duniani na katika hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano
huo alisema:-

"Tumeshindwa kuwazuia WANADAMU wasiende kwenye nyumba
za IBADA" Tumeshindwa kuwazuia wasisome VITABU vyao vitakatifu na kufahamu ukweli"
Tumeshindwa hata kuwazuia wasiwe na mapenzi ya kweli kwa MITUME yao " "Mara wapatapo muungano wa kweli kwenye MAHUBIRI ya DINI zao, mamlaka yetu yatakuwa yamefika mwisho."
Kwa hiyo kuanzia sasa waacheni waende kwenye nyumba zao za IBADA, waacheni waendelee na karamu zao za upendo,
LAKINI waibieni muda, ili wasipate nafasi ya kudumisha IBADA za kweli kweli kwa MOLA WAO MUUMBA...." 

"Hiki ndicho ninachotaka mfanye." Alisema Lucifer:
"wataabisheni WANADAMU WOOTE wasipate kamwe kushikamana na DINI zao na wasifungamane katika KUMCHA MUNGU" 
"
Tutafanyaje jambo hilo?" mashetani yalimwuuliza
kwa jazba.
LUCIFER aliwajibu:"hakikisheni wanakuwa 'BUSY' (BUSY= Being Under
Satan's York ) katika mambo yasiyokuwa na umuhimu katika
maisha yao na muwanzishie mipango mingi sana isiyohesabika ili
kujaza akili na ufahamu wao. "Washughulisheni na kutumia, na kutumia, na kutumia; na kukopa, nakukopa, na kukopa."
”Washawishini wake zao waende kufanya kazi kwa siku na kushinda huko kwa masaa mengi sana kwa siku na Waume
zao wafanye kazi kwa siku sita hadi saba kwa wiki, na masaa
10 hadi 12 kwa siku, ili wasiweze kupata nafasi ya kutulia na kutafakari chochote kulingana na mfumo huo wa maisha." "Wazuieni wasiwe na nafasi ya kukaa na watoto wao" 

"Wachocheeni zaidi akili na fahamu zao ili kuhakikisha
kwamba hawaiskii ile sauti ndogo tulivu ya Mungu wao." 
"Washawishini walize radio au kaseti au muziki kwenye simu,
popote wanapoendesha gari au wanapotembea kwa miguu.
Waache TV,VCR, CD na KOMPYUTER zikiwa zimewashwa kama kawaida majumbani mwao na mhakikishe kwamba kila duka na mgahawa kote duniani linapiga muziki usiokuwa wa KIDINI
tena mfululizo bila kukoma."  "Hii itasonga akili na fahamu zao
na kuvunja ule muungano kwa MOLA WAO."

"Jazeni magazeti na vijarida mbalimbali vya upuuzi kwenye
meza zao za kahawa na chai Duniani kote."

"Shindilieni habari na matukio mbalimbali ndani yafahamu zao
kwa muda wa masaa 24."  "Ingilieni kwenye muda wao wa
kuendesha barabarani kwa kuwaonyesha mabango na matangazo.'  "Kwenye masanduku ya posta na barua pepe jazeni vipeperushi
na majarida na kila aina ya matangazo ya habari za vitu na hudumu yanayowapa matumaini ya uongo."
"Wekeni wanawake warembo sana mitaani, club, maofisini  na kwenye Televisheni na majarida ili kwamba Wanaume walioko kwenye ndoa wadanganyike na kuamini kwamba urembo wanje ndio muhimu, na wasiridhike na wake zao."

"Wafanyeni wake zao wachoke sana wasiweze kuonyesha
upendo kwa waume zao nyakati za usiku.Wapeni maumivu
ya kichwa ili wasiwape waume zao upendo wanaouhitaji
sana,ili waanze kutazama kwingine. Wafanyeni Wanawake wawadharau Waume zao na kuwapuaaza.
"Hiyo itaparaganyisha familia zao haraka sana !
 
"Wapeni WANADAMU Waalimu wa uongo ili wawapotoshe wasifundishe maneno ya MUNGU ya kweli kwa watoto wao
na waumini wao." 
"Hakikisheni wanakuwa 'BUSY' na kusongwa na mambo kiasi kwamba hawapati muda wa kutafakari wema wa Mungu. Badala
yake wapeni kutalii kwenye maeneo ya ajabu, matukio ya
michezo, matamasha, kumbi za sinema na video."Wafanye wawe 'BUSY,' 'BUSY,' 'BUSY,! Yaani wasongwe na kusongwa na
kusongwa na kazi kwelikweli!" 
 
"Na wanapokutanika kwenye ibada zao za kiroho wafanye
waingie katika umbea na fitina na kuzungumzia  mambo
madogo madogo ya umbea na fitina ili waondoke wakiwa na dhamira mbaya zilizochafuliwa." 
"Jazeni visababishi vingi vya mambo katika maisha yao ili
wasiwe na nafasi ya kutafuta msaada na nguvu za MUNGU.
Muda si mrefu watakuwa wakitegemea akili zao wenyewe,
badala ya maelekezo ya MUNGU, huku wakihatarisha afya
zao na za familia zao kwa ajili ya maangamizi  yao wenyewe."
 "Itafanya kazi"  "Itafanya kazi!
"Huu ni mkakati kweli kweli. Mashetani yaliondoka kwenye
mkutano yakiwa na hamu kubwa sana ya kutekeleza majuku
hayo waliyopewa na kuanza kuwafanya WANADAMU wawe
wa kukimbia na mambo huku na huko. Watakuwa na muda
mdogo sana kwa ajili ya Mungu wao na familia zao. Wakakosa
muda wa kuwaeleza wengine kuhusu MAMBO YA IBADA na
kubadili maisha ya wanadamu.
NADHANI SWALI NI JE SHETANI AMEFANIKIWA
KATIKA MIPANGO YAKE HIYO? WEWE NDIYE HAKIMU !!!!!!!!
 
'UBIZE' au kutingwa na kazi kunamaanisha : kuwa chini ya mkataba au utumwa wa shetani?
PLEASE PASS THIS ON, IF YOU AREN'T TOO BUSY !!

Post a Comment

About This Blog

  © Blogger template Shush by Ourblogtemplates.com 2009

Back to TOP