Inawezekana. Powered by Blogger.

Inaendelea No 3

Wanaamini ni mchezo, na kuzimu ni mzaha, na wengi hawajui lolote juu yake. Ndiyo maana
nitakuonesha wewe huko kwa sababu wanaopotea ni wengi kuliko wanaoingia katika utukufu
wangu.” Aliposema hayo, niliona machozi yakitiririka kwenye vazi lake. Nikamwuuliza, “Bwana,
kwanini unalia?” Akanijibu, “Binti, kwasababu wengi wanaangamia, na nitakuonesha hii, ili
uende na uwaambie ukweli na wewe usirudie hapo.”
KUZIMU
Ghafla, alivyokuwa anaongea, kila kitu kikaanza kutembea. Ardhi ilitikisika na kupasuka, na
nikaona shimo jeusi tii chini.
Shimo:
Tulikuwa tumesimama kama kwenye mwamba na malaika wakituzunguka. Nikasema, “Bwana,
sitaki kwenda mahali huko!” akasema, “Binti, usiogope niko pamoja nawe.” Kwa sekunde chache
tukashuka kwenye shimo jeusi. Nilijaribu kuangalia lakini kulikuwa na kiza kikuu. Niliona duara
kubwa, na kusikia mamilioni ya sauti.
Nilipata moto. Nikajisikia ngozi yangu kuungua. Nikamuuliza, “Bwana, hiki ni nini? sitaki
kwenda mahali huko!” Bwana akasema hilo ni lango tu la kwenda kuzimu. Kulikuwa kuna harufu
mbaya, yakutisha, isiyovumilika, na nikamsihi Yesu asinipeleke mimi. Naye akajibu, “Binti, ni
muhimu ufike na kujua sehemu hii.” Nikalia, “Lakini kwanini, Bwana, kwanini?” naye akasema,
“Ili ukawaambie ukweli wanadamu; wanadamu wanaangamia, wanapotea na wachache sana
wanaoingia ufalme wangu.” (Mat.7:14) Akishasema hivi, hulia sana. Maneno yake yalinitia nguvu
na kunihimiza, kwa hiyo nikaendelea kutembea.
Ziwa la Moto:
9
Tulifika mwisho wa tanuru/lango, nilipoangalia chini niliona umati umefunikwa na miali ya moto. Bwana akasema “Binti, nakupa hii.” Ilikuwa ni faili kubwa lenye karatasi ambazo hazijaandikwa chochote. “Binti, chukua na kalamu hii ili uweze kuandika yote nitakayokuonesha, utakayoyaona na kusikia. Utaandika kila kitu ukionacho na utaishi nayo.” Nikasema, “Bwana, nitafanya, lakini nimeshaanza kuona mengi mno, Bwana. Ninaona roho zikiteswa, na kuzamishwa kwenye moto.”
Maxima:
Muda uliendelea kupita, na binti yangu alikuwa bado kalala pale. “Bwana, nini kinachotokea?” Machozi yalikuwa yakimtoka kwenye macho, lakini kila nilipomfuta, yalitoka tena. Nikaweka kioo mdomoni pake kuona kama anapumua, hakukuwa na pumzi. Tuliangalia mapigo ya damu, wapi, hakuna kitu!. Tuliweka mikono tumboni pake, wapi! Hakuna kitu. Mtumishi wa Bwana akasema, “mahali alipo sasa, siyo mahali pa kutabasamu bali mahali pa mateso.”
Angelica:
Nikamwambia Yesu, Nitashuhudia kuwa kuzimu ni halisi, kwamba ipo, lakini nitoe hapa sasa!” na akanijibu, “Binti, hatuja ingia bado mahali penyewe, na sijakuonesha chochote, tayari unataka nikutoe huku?” nikasema “Bwana, tafadhari nitoe mahali hapa,” tukaendelea kushuka kwenye korongo/shimo lakutisha! Nikaanza kulia na kupiga yowee, “Bwana, hapana, hapana, hapana, hapana……… Sitaki kwenda!” naye hujibu, “Unatakiwa kuona haya.”
Niliona mapepo yakutisha, ya kila aina, makubwa na madogo. Yalikuwa yanakimbia sana, na yameshika vitu mkononi. “Bwana, kwanini yanakimbia hivyo na yameshika nini?” akanijibu, “Binti, wanakimbia hivyo kwasababu wajua muda wao karibu kwisha, kwasababu muda wa kuwaharibu/kuwapoteza wanadamu, hususani watu wangu. Na walivyoshika mkononi ni mishale ya kuwaharibu wanadamu, kwasababu kila pepo amepewa jina na kwa kadri ya jina lake, ana mishale ya kumharibu mtu na kumleta huku kuzimu; malengo yao ni kumharibu mtu na kumleta kuzimu.” Na niliendelea kuona mapepo yakikimbia na kutoka kuelekea duniani na Bwana akaniambia; “Wanakwenda duniani ili kuleta na kuwatupa wanadamu huku." Alipokuwa akisema hivyo, Bwana hulia, hulia sana. Kila alipolia nami nililia pia.
Maxima:
Binti yangu alikuwa amekufa kwa masaa 23, lakini sikutoa taarifa kwenye mamlaka yoyote. Niliomba, “Bwana, nitasubiri kwa masaa 24. Kama binti yangu hatarudi ndani ya saa 24, nitampigia simu Daktari.” Lakini, Bwana alimrejesha kabla ya saa 24 hazijatimia.
Angelica:
Bwana akaniambia, “je uko tayari kuona nitakachokuonesha wewe?” Nikasema, “Ndiyo Bwana,”. Alinipeleka kwenye sero moja, ambapo nilimwona kijana akiwa matesoni katikati ya miali ya moto. Nikajulishwa namba sero yake, japokuwa sikuweza kujua ile namba, ilionekana kama imeandikwa kinyume hivi. Palikuwa na nembo kubwa mle ndani, na kijana alikuwa na namba 666 kwenye kipaji cha uso. Pia alikuwa na aina ya kipande cha chuma imebandikwa kwenye ngozi yake. Funza walikuwa wanamtafuna, haikuweza kuharibu kipande kile; wala moto haukuweza kukiunguza. Akapiga kelele, “Bwana, nirehemu mimi. Nitoe mahali hapa. Nisamehe mimi Bwana!” lakini Yesu alimjibu, “umechelewa, umechelewa sana: nilikupa fursa lakini hutaka kutubu.” Nikamuuliza Yesu, “Bwana, kwanini huyu yuko hapa?” mara nikajulishwa.
10
Akiwa duniani, kijana huyu alijua neno la Mungu, lakini ghafla akajitenga na Bwana na kuchagua
pombe, madawa ya kulevya na kupita katika njia zisizofaa. Hakutaka kufuata njia ya Bwana. Yesu
alimwonya mara nyingi juu la litakalompata. Yesu akasema, “Binti, yuko hapa kwasababu kila
anayeyakataa maneno yangu, anaye amhukumuye: lile neno nilisema naye litamhukumu siku
ya mwisho,” (Yohana 12:48) na Yesu akalia tena.
Bwana akilia, nitofauti nasi tuliavyo na zaidi yetu. Yeye hulia na maumivu makali moyoni na
uchungu usioelezeka. Bwana akasema, "Sikutengeneza kuzimu kwaajili ya wanadamu,”
Nikamuuliza, “Sasa Bwana kwanini wanadamu wapo huku,” Akanijibu, “Binti, niliumba kwajili
ya shetani na malaika zake, ambayo ni mapepo;(Mat. 25:41) lakini, kwasababu ya dhambi na
kukosekana kwa toba, wanadamu huishia hapa, na wengi wangamiao kuliko wanaofika katika
utukufu wangu!" Akaendelea kulia na huniumiza sana nimwonapo akilia. "Binti, nalitoa maisha
kwaajili ya wanadamu, ili wasiangamie, ili wasiishie hapa [Kuzimu]. Nalitoa maisha yangu kwa
upendo na huruma, ili wanadamu waendee toba na kuingia katika ufalme wa Mbinguni.” Yesu
kwa huzuni huugua kiasi cha kushindwa kustahimili maumivu, kadri aonavyo watu pale kuzimu.
Kwa kuwa na Yesu, kulinifanya nijisikie salama. Niliwaza, “kama nikimwacha Bwana aende,
ninge-nasa kuzimu pale” Nikamuuliza, “Yesu, je nina ndugu yangu mahali hapa?” Akanitazama
kwa jinsi nilivyokuwa nalia na akasema, “Binti, niko nawe,” Kwasababu nilikuwa mwenye hofu
sana. Akanipeleke kwenye sero nyingine. Sikuwahi kuwaza kumwona ndugu yangu kwenye sero
ile. Nilimwona mwanamke akiteswa, alikuwa na funza wakimla uso wake, na mapepo yakimchoma
mikuki mwilini. Naye hupiga kelele, “Hapana, Bwana, nihurumie, nisamehe mimi, tafadhari, nitoe
mahali hapa kwa dakika moja!” (Luka 16:24)
Kuzimu, watu huteswa na kumbukumbu za waliyoyafanya duniani. Mapepo hudhihaki watu na
kuwaambia, “abudu na kusifu kwasababu huu ndiyo ufalme wenu!” na watu hupiga kelele

11

Read more...

Mh!!!!!!!!!!!!!!!


Read more...

Chukua chako mapema


Mambo ya X-mass hawa walikutwa na mpiga picha wetu , wakiwa wanaondoka na sufuria kabisa baada ya kuona vyakula vimebaki vingi.

Read more...


Read more...

Madhara ya Mafuriko Dar



Kuna sehemu nyingine utadhani kulikuwa hakuna nyumba kabisa kwani zimesafishwa, Picha ya juu kabisa upande wa kulia kulikuwa na nyumba hapo lakini sasa imebakia msingi nyumba yenyewe haipo.

Read more...

Wajanja Mjini

Sikuhizi umezuka mtindo watu wanakufungia gari unaambiwa umeegesha (park) mahali sipo lakini hiyo sehemu uliyo egesha gari lako (parking) haina maelezo yoyote kuhusu hairuhusiwe. Hawa jamaa wameungana na watu wa halmashuri ya Ilala na kuwachukulia hela zao. Usikubali kulipa sehemu isiyokuwa na maelekezo kuhusu hiyo sehemu. Kisheria kunatakiwa kuwe na kibao cha kutoa maelekezo.

Read more...

Bongo imebaki sheria moja tu HAKUNA SHERIA

 Huyu mwenye gari yeye baada ya kuona kuna foleni kubwa akaamua kupita upande asio ruhusiwa. Lakini hii imekuwa kwa hapa Dar ni kama kitu cha kawaida maana inafanyika hata mbele ya Polisi wa usalama barabarani.

Read more...

Inaendelea No 2

aliyepo akinitazama. Wakaniona jinsi nilivyobadilika toka unyonge na kuwa mwenye furaha.
Nilikuwa natabasamu, narukaruka na kuimba.
Picha wakimwombea:
Maxima:
Binti yangu ghafla akawa mwenye furaha ndani ya moyo na kuanza kula. Alionja karibia kila kitu
kilichokuwepo, huku akisema, “Kama sitarudi, sawa nimeshakula na kushiba.”
Angelica:
Kila mmoja akaanza kucheka na kuuliza, “kwanini uko hivyo badala ya kuwa na huzuni, unafuraha
na mwenye raha?” nikawajibu, “Ndiyo ninafuraha: ninakwenda kumwona Bwana, nitakuwa naye,
lakini sijui kama nitarudi. Kwa hiyo nataka kugawa vitu vyangu vyote.” Wote wakastaajabu na
kuniuliza, “Unataka kugawa vitu vyako vyote?” macho ya mama yangu yalinitazama kwa
mshangao zaidi!
Maxima:
Binti yangu akaanza kugawa vitu vyake. Aligawa vyote, vyote! Ma-dada wa kanisani walikuwepo,
nao pia aliwapa baadhi ya vitu kwa kila mmoja. Nilipomuuliza nia yake, alisema, “Kama nikirudi,
watanirejeshea vyote, lakini nisiporudi, watabaki navyo.”
Angelica:
Niliwaza huzuni aliyokuwa nayo mama yangu niliposema maneno hayo. Lakini nilijisikia furaha
tupu, kwa hiyo nikaendelea kugawa vitu: nguo, kitanda, simu ya mkononi, kila kitu, lakini kwa
sharti: kama nikirudi, kila kitu kitarejeshwa kwangu. Wote wakaanza kucheka.
Maxima:
Binti yangu alikuwa na msimamo na nia ya dhati, lakini kama mama nilishikwa na huzuni sana.
Haikuwa jambo rahisi. Niliwaza, “Bwana muda huo ukiwadia, itakuwajekuwaje?” Sikuweza
kuelewa. Na walipoanza kuomba, nilikuwa napanga vitu ndani ya nyumba. Walisema, “Dada njoo
tuombe.” Lakini niliwajibu, “Nyie endeleeni, nitajiunga nanyi muda si mrefu. Ngoja nimalizie kazi
hii.”
Angelica:
Wote walikuwa wananiangalia mimi tulipokuwa tunaomba. Niliomba, “Bwana, nataka kufanya
mapenzi yako. Wewe si mwanadamu hata useme uwongo au ujute, najua wewe ni mkweli. Kama
nitakuaibisha, basi vema unichukue moja kwa moja; lakini kama nitayafanya mapenzi, basi
unirejeshe tena, lakini nisaidie kusema ukweli, niandae mimi, nisaidie kuhubiri na kuwaambia watu
kutubu.” Hiyo ndiyo ilikuwa sala yangu fupi sana. Nilimwambia mtumishi wa Bwana,
6
“Usimwambie mama yangu maneno niliyomwomba Bwana.” Naye akajibu, “sitamwambia sasa,
lakini mara Bwana atakapokutwa, nitamwambia.” Tuliendelea kuomba na kuungana katika duara.
Maxima:
Ilipofika saa 9:30 jioni, Bwana akamwambia mtumishi wake ampake mafuta binti yangu. Kwa hiyo
baadhi yetu tulikwenda chumbani na kumpaka mafuta. Alitupa dakika mbili tumpake mwili mzima,
toka kichwani hadi chini, kila mahali, mwili mzima. Akawa mwili wote amepakwa mafuta.
KIFO CHAKE
Angelica:
Mama yangu na dada mmoja, Fátima Navarrete, walinipaka mafuta. Kadri walivyokuwa
wananipaka, nilijisikia kama kuna kitu kinanifunika, kama kioo kilinizunguka mimi. Ni vigumu
kuelezea, nilijisikia kama nimezingirwa na ngao fulani, na nashindwa kuelezea nilivyokuwa
najisikia. Baada ya hapo kila walipojaribu kunigusa walishindwa!
Maxima:
Kadri tulivyokuwa tukimwombea Angelica, nilijaribu kuweka mkono juu yake, nilishindwa!
Alikuwa amezingirwa na kitu. Ilikuwa ajabu, hakuna aliyeweza kumgusa tena! Uzio huo ulianzia
kichwani hadi miguuni, karibia sentimenta 30 (Inchi 12). Hilo lilinitisha zaidi mimi. Nimewawekea
mikono wengi kabla, katika huduma ya Bwana, lakini jambo kama hili halijawahi kutokea!
Nikasema, “Oh, kuna jambo lazima linatendeka,” na nikaanza kuomba na kumshukuru Bwana.
Ghafla, nikasikia furaha kubwa sana. Huzuni iliyokuwa moyoni ikanitoka, maumivu yakakoma na
sasa nikasikia raha na furaha ajabu! Tuliendelea kuomba na ilipofika saa 10.00 jioni, binti yangu
akaanguka sakafuni.
Angelica:
Wakati wa maombi, nilisikia kuishiwa pumzi; nikashindwa kupumua. Nikasikia maumivu tumboni
na moyoni. Nilijisiki damu ikisimama, na ghafla maumivu makali mwili mzima. Nililoweza
kusema, “Bwana, nipe nguvu, nipe mimi nguvu!” kwasababu nilijisikia kushindwa kuendelea zaidi.
Sikuwa na nguvu kabisa, zote zilinitoka! Na nilipoangalia juu mbinguni, katika roho, si kwa macho
ya mwilini, niliona mbingu zikifunguka. Niliwaona malaika, siyo wawili au kumi, bali kwa
mamilioni wakiwa pamoja wamekusanyika. Katikati yao niliona mwanga, mara 10,000 zaidi ya
jua. Na nikasema, “Bwana ni wewe unayekuja!”
Maxima:
Alipoanguka chini, tulijaribu kumsimamisha, lakini hakuweza kusimama mwenyewe. Muda huu
tuliweza kumgusa. Alikuwa akisema, “Omba. Sina nguvu, mama, sina nguvu na ninasikia
maumivu.” Mwanzo alisikia maumivu tumboni, na baadaye moyoni. Tuliendelea kuomba na
kumsihi Bwana. Bwana alichukua maisha yake!
Picha Mwili wake:
7
Sijawahi katika maisha yangu kumwona mtu akifa. Nilishuhudia binti yangu, akigugumia maumivu! Haikuwa rahisi hata kidogo! Sikuweza kuelewa maneno yake ya mwisho, na mwisho alitulia. Niliweka mikono yangu usoni pake, na kioo mdomoni kuona kama alikuwa anapumua. Hakuwa na pumzi tena, alitulia kimya kabisa. Nilimshika, alikuwa angali na joto kama kawaida. Nilichukua shuka na kumfunika na kwa muda mfupi akaanza kupoa na kuwa wa baridi sana. Nywele zake zikalala, kama za maiti na akabadilika ubaridi wa barafu.
Angelica:
Yesu alikuwa anashuka chini, na nikajisikia mwili ukifa. Kadri Yesu na malaika walivyozidi kukaribia, nikajisikia kuondoka, na sikuwa mimi tena. Sikuwa hai tena, nilikuwa nakufa na kugugumia maumivu! Wakati mwili wangu ulipoanguka chini, walikuwa tayari wamefika. Nyumba yetu ilijaa malaika, na katikati yao niliona mwanga mkali kuliko wa jua! Ilikuwa vigumu; nilisikia maumivu makali wakati roho yangu ilipotenganishwa na mwili. Nilikuwa nalia na kupiga kelele, kadri nilivyoona mwili wangu sakafuni. Nilimuuliza, “Bwana, nini kinachotokea? Nini kinachotokea?” Nilijaribu kuugusa mwili wangu na kuurudia tena, lakini nilipojaribu, ilikuwa kama kushika hewa: sikuweza kuugusa, mkono wangu ulipitiliza. Hakuna kati ya waliokuwa wananiombea aliyenisikia! Na nikapiga kelele, “Bwana, nisaidie mimi!”
Maxima:
Mume wangu alifika tulipokuwa tunaomba, na alimkuta pale. Bwana alinipa nguvu kwa kuwa sikujua la kufanya. Ilikuwa kama vile yuko mahututi (kwenye coma), lakini nilijua yuko salama, kwasababu ilikuwa ni kazi ya Bwana. Kwahiyo nikasema “Bwana, mapenzi yako yafanyike.”
BWANA YESU KRISTO
Angelica:
Wakati huo nasikia sauti ya Bwana, sauti nzuri kama radi lakini ya UPENDO, “Usiogope, Binti, kwa kuwa mimi ni Yehova, Mungu wako, na nimekuja hapa kukuonesha niliyokuahidi wewe. Inuka, kwa kuwa mimi ni Yehova, ninayekushika mkono wako wa kuume na kukuambia, usiogope, nitakusaidia wewe." Ghafla, nikasimama. Nilikuwa nimepiga magoti chini, ninauangalia mwili wangu, nikitaka kuurejea bila mafanikio. Niliposikia sauti yake, woga ukanitoka, na sikuwa na hofu tena. Nilipoanza kutembea, malaika wakaanza kufungua njia. Kulikuwa na mwanga mkali ung’aao, na nilipouangalia nilisikia amani ya ajabu. Kadri nilivyoangalia, nilimwona mwanaume mzuri, mrefu, aliyevaa vizuri na kuvutia sana kumwangalia, mwenye siha njema. Mwanga ulitoka kwake. Kulikuwa na mwanga mkali kiasi cha kushindwa kumwangalia uso wake! Lakini niliweza kuona nywele zake za dhahabu ing’aayo na vazi jeupe na mshipi kifuani pake. Ukisomeka, “MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA.”
Nilimwangalia miguuni pake, alikuwa amevaa sandozi zenye mng’ao wa dhahabu, dhahabu safi. Alikuwa mzuri sana! Akaninyooshea mkono wake. Nilipomshika mkono wake, haikuwa kama nilipojaribu kuugusa mwili wangu, mkono haukupitiliza. Nikauliza, “Nini kinachotokea?” naye akasema, “Nitakuonesha wewe kuzimu ili ukirudi uwaambie wanadamu kuwa kuzimu ni halisi; kuwa ni kweli ipo. Na pia utukufu wangu nitakuonesha wewe, ili uwaambie watu wangu wajiaandae, kwa kuwa utukufu wangu ni halisi na mimi pia.” Akasema, "Binti, usiogope” akarudia kusema tena na mimi nikasema, "Bwana, nataka tu kwenda Mbinguni, lakini siyo kuzimu, kwasababu nimesikia kunatisha!” Akasema, “Binti, nitakuwa nawe. Sitakuacha huko na nitakuonesha huko mahali kwasababu wengi wanajua kuzimu ipo lakini hawaiogopi.
Itaendelea

Read more...

Wacha weeeee

Read more...

Read more...

Read more...

Haya wakati wa kuchangamsha viungo


Read more...


Read more...





Read more...

Keki Time

Read more...

Read more...

JIANDAE MH!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Yakutisha na Kufurahisha

JIANDAE KUKUTANA NA MUNGU WAKO!
FALME ZA MBINGUNI NA KUZIMU,
NA KURUDI KWA KRISTO
NA
Angelica Zambrano
Imefasiriwa na Alpha Wilson Magubila kwa Neema aliojaliwa na Mungu
Kwa kipindi cha masaa 23, binti mdogo wa ki-Ecuado aitwaye Angelica alioneshwa falme za
Mbinguni na Kuzimu, na kurudi kwa Kristo mara ya pili. Alishuhudia Yesu akilia kwa huzuni
aonapo umati wa roho zilizopotea milele, ulimwengu uliomkataa yeye, kanisa lisilo tayari kabisa
kwa ujio wake, watu wameacha kushuhudia kwa walipotea mbali na kweli, na anasa za dunia
zimeteka hata watoto kwa shetani. Alishuhudia watu maarufu wakiteswa katika moto, waimbaji,
wanamuziki na hata Papa. Angelica alioneshwa jinsi ufalme wa Mbinguni ulivyoandaliwa kwa
uzuri na utayari, utukufu usioweza kufikirika, ambapo hakuna uovu. Japokuwa Yesu anakuja kwa
ajili ya watakatifu tu; wengi wa wana wa Mungu hawatakuwa tayari kwa siku ile, na wataachwa
nyuma katika ulimwengu utakaogawanyika vipande vipande. www.DivineUfunuo.info/23 (Mahojiano
kwa video, mwanzoni ni kwa lugha ya Kihispania, huko El Empalme, Ecuador. Sept. 29, 2009).
Maxima (Mama yake Binti):
Jina langu ni Maxima Zambrano Mora, tunasali kanisa la "Casa de Oracion" huku El Empalme.
Tulikuwa katika kufunga kwa siku 15, na kulia kwa Mungu. Binti yangu Angelica aliungana nasi
pia. Katika kipindi hicho cha siku 15 cha kufunga, niliweza kupata maono zaidi ya asili, ambayo
sijawahi kuona kabla. Tulikuwa tunaomba na kufunga katika kipindi maalumu cha kumtafuta
Bwana, tuliendelea kuomba na kulia pale nyumbani, tukisubiri Mungu aseme nasi.
Bwana alitutia matumaini makubwa sana. Kwaajili ya majaribu yetu tulikaribia kukata tamaa,
lakini Bwana alikuwa pamoja nasi kutusaidia. Alitupa neno la Yeremia 33:3 "Niite, nami
nitakuitikia, ame nitakuonesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.” Binti yangu alitia
msisitizo sana katika neno hili kwa Bwana, japokuwa sikujua kwa wakati huo.
2
Angelica (Binti Mhusika):
Jina langu ni Angelica Elizabeth Zambrano Mora. Nina umri wa miaka 18, na ninasoma chuo cha
"Colegio José María Velazco Ibarra",
hapa El Cantón, El Empalme, Ecuador. Kwanza nilimpokea Kristo nilipokuwa na umri wa miaka
12, lakini nalijiambia mwenyewe, "Hakuna hata mmoja wa rakifi zangu aliyeokoka na nikajisikia
aibu miongoni mwao", kwa hiyo nirudi nyuma mbali na Mungu na kuishi maisha mabaya. Lakini
Mungu alinivuta nitoke huko.
Siku ya sherehe ya kutimiza miaka 15, nirejea tena kupatana na Bwana, lakini nia haikutulia sawa
sawa. Biblia inasema (Yakobo 1:8), "Mtu wa nia mbili husita-sita katika nia zake zote" na mimi
nilikuwa sawa na mtu huyu. Baba yangu aliwahi kusema "Hutakiwi kuwa hivyo, siyo vizuri, ni
vibaya mwanangu" lakini nalimjibu, "Hivi ndivyo nilivyo, nataka kuwa hivyo, hakuna mtu wa
kuniambia namna nitakiwavyo kuwa, wala chakufanya, wala namna ya kuvaa, au mwenendo."
Naye alijibu, "Mungu atakushughulikia na atakubadilisha wewe."
Siku ya sherehe ya kutimiza miaka 17, nilimkaribia Bwana. Tarehe 28 mwezi Aprili nilimwendea
Bwana na kumwambia, "Bwana, nijisikia vibaya sana, najua kuwa mimi ni mwenye dhambi” na
nilimweleza jinsi ninavyojisikia. "Bwana, nisamehe mimi. Natamani uandike jina langu katika
kitabu cha Uzima na unipokee niwe mwanao." Nilitubu na kutoa maisha yangu kwa Bwana rasmi.
Nikasema “Bwana, naomba unibadilishe, ufanye tofauti ndani mwangu." Nililia kwa moyo wangu
wote, huku nikimwomba Bwana anibadilishe mimi. Lakini kwa kadri ya muda ulivyozidi kupita,
sikuona madiliko yoyote. Badiliko pekee nikuwa nilianza kuhudhuria kanisani, kusoma biblia na
kuomba. Hayo tu ndiyo mabadiliko katika maisha yangu.
Ilipofika mwezi Agosti, nilikaribishwa katika mfungo wa siku 15. Niliamua kushiriki, lakini kabla
ya kuanza nilisema: “Bwana, naomba unishughulikie hapa." Katika kipindi chote cha mfungo,
Bwana alikuwa anasema na karibu kila mtu, kasoro mimi tu! Ilikuwa kama vile Bwana hajaniona,
na hilo liliniumiza sana. Nikaomba, "Bwana, hutanishughulikia mimi?" Nikaomba na kulia peke
yangu na kusema tena, "Bwana, je unanipenda? Je upo hapa? Upo nami hapa? Kwanini husemi
nami kama unavyosema na kila mmoja hapa? Unasema mambo mengi kwa wenzangu, hata maneno
ya unabii, lakini siyo kwangu" Nilimwomba ishara ya kuwa yu nami, na Bwana akanipa neno la
Yeremia 33:3, "Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonesha mambo makubwa, magumu
usiyoyajua." Nikasema, “Bwana, je umesema nami?” Kwasababu nilisikia sauti yake na kupata
maono ya maneno yaliyoandikwa katika Yeremia 33:3.
Nikasema “Bwana, hiyo ni kwaajili yangu?” Nilitunza na kukaa nalo kimya mwenyewe wakati kila
mmoja akishuhudia waliyopewa na Bwana na kuoneshwa. Lakini mimi nilitunza siri yangu na mara
kwa mara nilijikumbusha na kutafakari maneno: " Niite" maana yake nimwombe, lakini nini maana
ya: "mambo makubwa, magumu" niliwaza, “Huenda ikamaanisha Mbinguni na Kuzimu." Kwa
3
hiyo nalimwambia “Bwana, naomba unioneshe Mbinguni tu, lakini siyo kuzimu, kwasababu nimesikia kuzimu ni sehemu ya kutisha na mbaya sana." Lakini baadaye nikaomba kwa moyo wangu wote, "Bwana kama ni mapenzi yako kunionesha, na iwe hivyo, lakini nibadilishe kwanza. Naomba ufanye tofauti ndani mwangu, nataka kuwa tofauti.”
Tulipomaliza kufunga, kulikuwa na majaribu na vipindi vigumu na mara nyingine nalijisikia kuishiwa nguvu, siwezi tena kuendelea na Bwana. Lakini alinipa nguvu. Nilianza kusikia sauti yake na kumjua vema zaidi. Tukawa marakifi wazuri. Bwana ni rafiki yetu mwema, na Roho Mtakatifu pia. Niliwahi mwambia, "Bwana, wewe ni rafiki yangu bora. Nataka kukujua vema," na nilishirikiana naye katika mawazo yangu yote.
Nilimwomba kipindi chote cha mwezi Agosti hadi Novemba, na mtumishi wa Bwana akaja nyumbani kwetu na kusema, "Bwana akubariki." Nikajibu, "Ameni." Kisha akasema, "Nimekuja kukuletea ujumbe toka kwa Mungu…...Jiandae, kwasababu Bwana atakuonesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Atakuonesha wewe Mbinguni na kuzimu kama ulivyokuwa unamwomba neno la Yeremia 33:3." Nikamwuliza, "Ndiyo, lakini umepataje kujua? Sijamweleza yeyote." Akanijibu, "Mungu unayemtumikia na kumsifu, ndiye nimsifuye, alinieleza kila kitu."
Mara tukaanza kuomba. Baadhi akina dada toka kanisani kwetu na wana familia wangu wakaungana nasi kuomba. Lakini mara tulipoanza kuomba, nilianza kuona Mbingu zikifunguka. Mara nikasema “naona mbingu zikifunguka, na malaika wawili wanashuka kuja tulipo" Mtumishi wa Mungu akasema “waulize kwanini wamekuja hapa”
Walikuwa warefu na wazuri wakupendeza; wana mbawa nzuri. Walikuwa wakubwa na wenye kung’aa, na walionekana wakiangaaza, mng’ao kama wa dhahabu. Walivaa sandozi za vito vya thamani na walivaa mavazi matakatifu. "Kwanini mko hapa?" Wakatabasamu na kusema, "Tupo hapa kwasababu tuna kazi yakufanya….. tupo hapa kwasababu unatakiwa utembelee Mbinguni na kuzimu na hatutaondoka mpaka yote yatakapo pita." Nikawajibu “safi sana, lakini mimi natamani kutembelea Mbinguni tu, siyo kuzimu” Wakatabasamu na kuendelea kuwepo na hawakusema lolote zaidi. Baada ya kumaliza maombi, niliendelea kuwaona wakiwepo.
Pia nilianza kumwona Roho Mtakatifu; ni rafiki yangu bora; ni Mtakatifu, amejaa pote na yuko kila mahali wakati wote. Ninamwona, anaangaza na kung’aa sana, naona tabasamu lake na mtazamo wake wa upendo! Ni vigumu sana kumwelezea, kwa sababu ni mzuri zaidi ya malaika. Malaika wana uzuri wao lakini Roho Mtakatifu ni zaidi sana kwa yote. Naweza kuisikia sauti yake, sauti ilijaa upendo na matulizo makuu. Siwezi kuelezea kabisa sauti yake; kama radi si radi wakati huo huo yakuvutia. Yeye husema “Niko pamoja nawe” Kwa hiyo nalijitahidi kuendelea kutembea na Mungu, japo majaribu yalizidi kutuzingira. Tulikuwa tunapita kipindi kigumu sana, lakini chenye ushindi waajabu. Mie husema “Bwana, mapenzi yako yatimizwe.” Niliendelea kuwaona malaika wale hata nikiwa shule na pia darasani. Nilikuwa mwenye furaha ajabu kwa sababu niliwaona vema.
Mtumishi wa Bwana, aliyetutembelea, aliniambia nijiandae, kwa sababu nitakwenda kuona Mbingu na kuzimu. Lakini pia aliniambia kitu kigumu. Alisema “Nitakufa.” Haikuwa rahisi niliposikia neno hili.
4
"Nitakufa namna gani? mie mdogo sana", Nilimuuliza. Akanijibu, “Usihofu juu ya lolote, Kila kitu Mungu afanyacho hakina makosa wala mawaa, na atakurejesha duniani, ili utoe ushuhuda juu ya Mbinguni na Kuzimu, kwakuwa hilo ndilo Bwana anataka sote tujue” Nikasema “Amen, lakini nitagongwa na gari au nitakufaje?” Mawazo yalinisonga sana, lakini Bwana akaniambia nisihofu, kila kitu kiko katika uwezo wake. Nikasema, “Ahsante Bwana”
Ilipofika tarehe 6 Novemba, baada ya kurejea nyumbani toka shule, malaika wale walikuwa nami, hata nilipokuwa namsifu Bwana. Wao walikuwa hawaongei nami; bali walidumu kusema, “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Hallelujah," huku wakimpa utukufu, heshima na sifa Baba wa Mbinguni. Roho Mtakatifu pia alikuwa na malaika wale huku akifurahi. Watu wengi husema injili/ wokovu ni wa kuchosha/kukera, lakini huo ni uongo mkubwa toka kwa mwovu ili kuwafanya watu wasitafute uwepo wa Mungu. Nami pia niliamini hivyo hapo kwanza, lakini baada ya kukutana na Bwana na Roho Mtakatifu, najua injili haikeri wala kuchosha, niburudisho la ajabu hapa duniani!
Ninaweza kumwona; kucheza na kuongea naye Roho Mtakatifu. Lakini malaika walikuwa hawaongei nami, ila walikuwa wakimsifu Bwana. Nikimwambia Roho twende nami nakufanya hili na lile huja na kuwa nami. Ninaweza kujihisi na kumwona vema.
Japokuwa wengi hawamwoni, yeye yupo! Mahusiano haya yamendelea, hata hakuna sababu ya kuyasimamisha, hasa baada ya kuonja radha yake na faida za Roho Mtakatifu…… hakuna njia ya kujitenga naye jinsi alivyo mwema na wafaida, hasa nikikumbuka alikonitoa, jinsi nilivyokuwa, ninamshukuru sana kwa rehema zake na upendo wake kwa wanadamu na kwangu mimi!
Tarehe 7, Novemba, nilipokuwa narudi nyumbani, nikasikia sauti ikisema “Jiandae, kwakuwa leo utakufa,” Nilijua kuwa ni Roho Mtakatifu kwa vile nilimwona vema. Niliipuuza sauti yake na kusema “Bwana, Sitaki kufa leo!” Lakini alirudia, “Jiandae, kwakuwa leo utakufa!” Mara hii sauti ilikuwa ya juu zaidi na mkazo mkubwa. Nikajibu, “Bwana, najua ni wewe unayesema nami; nimeuliza ili kupata uhakika tu, mapenzi yako yatendeke. Nitafanya kila utakalo niambia, najiachia kwako Bwana, japo naogopa, najua upo nami, nawe ni wa kweli.” Niliomba, “Bwana, Yule mtumishi wako uliyemtumia kunipa ujumbe mara ya kwanza, mlete muda huu, nimkute nyumbani, na umpe tena neno hili aseme nami kuwa leo ndiyo siku yangu ya kufa.” Sasa mara zote Bwana hujua ya nyuma, yaliyopo na yajayo. Alijua kuwa nitamwomba neno hili. Kwa hiyo nilipofika nyumbani nikamkuta mtumishi wa Bwana ameishafika!.
Maxima (Mama ya Binti):
Binti yangu alipofika nyumbani, tulikuwa jikoni. Mara Angelica alipomwona mtumishi wa Bwana, akasema, “Bwana akubariki.” Mtumishi wa Mungu akajibu, “Bwana akubariki nawe. Je uko tayari? Kwa kuwa leo ndiyo siku Bwana atakayo kuchukua, saa kumi jioni.” Angelica alisimama na kushikwa na mshangao kwamba Bwana amejibu ombi lake na kufanya vilevile alivyomwomba njiani.
Angelica:
Niliposikia hayo maneno ya mtumishi, nikasema, “Ameni... lakini sitaki kufa, sitakufa! Hapana, Bwana, naogopa, naogopa sana, ninahofu kubwa!” Mtumishi wa Bwana akasema, “Tuombe ili hofu ikutoke sasa kwa jina la Bwana.” Nikasema, "Ameni" na tukaomba. Ghafla nikajisia hofu yote imenitoka na furaha isiyoelezeka ikajaa ndani mwangu, nakuanza kuwaza kuwa kifo ni kitu chema kuliko vyote nikitamanicho kinifike! Nikanza kutabasamu na kicheka wakati huo kila mmoja
Itaendelea siku inayofwata

Read more...

BMW

Read more...

Read more...

Mama na Mwana wamependeza

Read more...

Read more...

Read more...

Read more...

Read more...

Mdada

Read more...

Jamaa huyu na Mke wake waliamua kuja kanisani wakati watu wanatoka ndiyo hivyo tena mambo ya sherehe.

Read more...

Mdada mwenyewe kwenye pozi kanisani

Read more...

Read more...

Wakati wa zawadi kanisani kwa vijana.

Read more...

Read more...

Read more...

Mama na Mwana wamependeza

Read more...

Read more...

Mambo ya Mibarikio hayo bongoland




Familia ya Dk J N ikiwa kanisani kwenye kipaimara huko Kunduchi

Read more...

Sabuni ya Mmbono

Hizo ndizo sabuni za jatropha (mmbono), zimetengenezwa na mafuta yatokanayo na mbegu za jatropha (mmbono), mmea wa mmbono. They are very nice ones, makes you soft and clean, if you have a rough skin i recommend you try them, na kama unakuaga na ngozi kavu ndio kabisa they provide a solution, now zinapatikana mwenge madukani yale yanayoangaliana na kituo cha mabasi ya tegeta au tuwasiliane kwa email ndeonasia@yahoo.com. Zinafaa na kwa watoto pia, kwa ngozi nzuri na yenye afya, si unajua tena zinatengenezwa na mafuta ya mbegu za jatorpha,ambayo ni mafuta mazuri sana. Hazina chemicals and they are not perfumed. Magonjwa ya ngozi, muwasho, kila kitu maliza kabisa, just give them a try and tell the world. Wasiliana nasi kwa Simu Namba
+255785 298 679
e-mail ndeonasia@yahoo.com
Karibu sana.

Read more...


We are an importer/exporter company based in the United Kingdom with global dealings.Cars & Trucks,Parcels,ContainersHospital Equipment
Personal Effects Domestic Goods  and Packaging of dedicated Goods.
Plants & Machinery.
We Collect goods and equipment throughout the UK but for Europe we can facilitate.
CONTAINERS PRICE  


       20 ’ To Dar Es Salaam    £1,450
40’ To Dar & Mombasa     £2,150

     Saloon to Dar/Mombasa  730
4X4 to Dar/Mombasa  800
Trucks from $81.50 per cubic metre
(Length X Width X Height ) Metre

We specialise in Forwarding  to East Africa,West Africa ,Middle East and USA and ESAC Ltd provide clearing goods if require to Tanzania.
--
 NOTE:WHEN U INTRODUCE A FRIEND YOU GET A DISCOUNT. 
Regards,
 
Operations Manager: Mndima Fue
Eastern & Southern Africa Cargo Limited (ESAC)
(Exporters & Importers )
Tel No:             +44 783 369 2695      ,             +44 0148 221 4949       (North England - HQ)
Tel No:             + 44 118 954 5890      ,             +44 79000 43224       (South England office)
  132 Victor Street, HULL, HU9 2EY- East Yorkshire
REG NO:07609023. VAT NO:113 999 585

Read more...

Kipa Imara hapo maeneo ya kawe




Watoto wakiwa kwenye sherehe ya kipa imara iliyofanyika mwisho wa wiki hapo Kawe

Read more...

About This Blog

  © Blogger template Shush by Ourblogtemplates.com 2009

Back to TOP